OMMS YASAINI MAKUBALIANO NA TAASISI YA LAWS.AFRICA

Imewekwa: 13 Jul, 2023
OMMS YASAINI  MAKUBALIANO NA  TAASISI YA LAWS.AFRICA

DODOMA-Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  leo ( alhamisi) imesaini  Makubaliano ( MOU)   baina yake na  Taasisi ya LAWS.AFRICA.

Hafla ya  utiaji Saini  wa  makubaliano hayo imefanyika katika siku ya kwanza ya Warsha ya siku mbili  kuhusu  utoaji na upatikanaji endelevu wa  sheria  kwa njia ya Kijiditali. Warsha hiyo imefunguliwa na  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damasi Ndumbaro

Akizungumza na  mwandishi wa Habari hizi mara baada ya  kusaini makubalino hayo kwa niaba ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikalia, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Dkt. Evaristo Longopa amesema,  Makubaliano hayo  yanahusu ushirikiano kwenye masuala ya kuwezesha Sheria zinatotungwa na Bunge na  sheria ndogo kupatikana kwa urahisi  kwa njia za kijiditali.

Dkt. Longopa amebainisha kwamba makubaliano  hayo  yataongeza na kuboresha utekelezaji wa majukumu ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  hasa katika  kuhakikisha kwamba sheria ambazo zimefanyiwa urekebu  na zile ambazo zimefanywa tafsiri kwa lugha ya kiswali zinawafikia wananchi kwa urahisi na wakati  wowote.

“makubaliano  haya yatutasaidia sana  siyo tu kuhakikisha kwamba sheria  zinapatikana kwa urahisi kwa njia ya kidijitali lakini pia zinapatikana  zikiwa na marekebisho yote yaliyofanyika”  akasema  Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Na kuongeza  kuwa  makubaliano hayo yatahusu pia kubadilishana  uzoefu na uwezeshaji  kwa njia  ya mafunzo  katika Chuo Kikuu cha  CAPE- TOWN.

Aidha  Pamoja  na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  kusaini  makubaliano nayo vilevile  Tume ya Kurekebisha Sheri nayo imesaini   Makubaliano hayo.

Warsha hiyo  ya siku mbili  imeandaliwa na  GIZ, African Lii na LAWS . AFRICA  na washiriki wake ni  Mahakama ya Tanzania, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Seriali,  Tume ya Kurekebisha Sheria,  Chama cha Wanasheria wa Tanganyika ( TLS) Ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa Seriali na Wizara ya Katiba  na Sheria.

Ajenda au mada kuu  ya  Warsha hii ni  utoaji endelevu wa sheria za Tanzania kupitia   mifumo ya Kidijitali.