Mikataba na Makubaliano

Divisheni hii ni  moja ya Divisheni Tatu (3) za Kisheria  katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Kazi zake za msingi ni  kutoa ushauri na kuendesha  majadiliano kwa niaba ya Serikali katika Mikataba yote. Idara inaongozwa na  Mkurugenzi pamoja na Wakurugenzi wasaidizi.

Majukumu ya Divisheni ya Mikataba

  • Uhakiki wa Mikataba ya Manunuz.i
  • Uhakiki wa Makubaliano ya Kitaifa na Kimataifa.
  • Kuhudhuria na  kutoa mapendekezo ya Nchi katika Vikao vya Kikanda na Kimataifa kwa maslahi ya Nchi.
  • Kuhudhuria Vikao vya Majadiliano ya Mikataba mbalimbali yenye maslahi kwa nchi kila inapohitajika.
  • Kutoa Ushuri kwenye Mikataba ya Mikopo.

Sehemu za Divisheni ya Mikataba

Divisheni hii ina  Sehemu Tatu (3) zinazoongozwa na  Wakurugenzi Wasaidizi. Sehemu hizo ni :-

  1. Sehemu ya Mikataba ya Ununuzi wa Umma
  2. Sehemu ya Mikataba ya Makubaliano ya Kimataifa
  3. Sehemu ya  Mikataba ya Uwekezaji, Maliasili na Fedha.