Uandishi wa Sheria

Divisheni hii  ni  kati ya  Divisheni Tatu za Kisheria katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Kazi za msingi za Divisheni hii ni  kuandaa na  kuandika Miswaada ya Sheria  zote zinazotungwa na Bunge na Sheria ndogo zinazotungwa na Mamlaka mbalimbali. Divisheni pia inahuka na  kutafsiri sheria kutoka lugha ya  Lugha ya Kiingereza kwenda Lugha ya Kiswahili. Divisheni  hii pia inalojukumu la  kufanya urekebu  wa sheria zote za nchi. Idara inaongozwa na Mkurugenzi na Wakurugenzi Wasaidizi.

Majukumu ya Divisheni ya Uandishi wa Sheria

  • Uandaaji wa Miswaada ya Uandishi wa Sheria
  • Tafsiri ya Sheria kutoka lugha ya  Kiingereza kwenda  lugha ya Kiswahili
  • Urekebu wa Sheria
  • Kuhudhuria Vikao vya Kikanda na Kimataifa vinavyohusu uandishi wa Sheria kila inapohitajika na kutoa ushauri wa Kisheria.

Sehemu za Divisheni ya Uandishi wa Sheria

  1. Sehemu ya Uandishi wa Sheria
  2. Sehemu ya Urekebu wa Sheria
  3. Sehemu ya Fasiri ya Sheria